Mhubiri Mlango 3 Ecclesiastes
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;
Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?
Mhubiri 3:10 Ecclesiastes 3:10
Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
Mhubiri 3:11 Ecclesiastes 3:11
Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
Mhubiri 3:12 Ecclesiastes 3:12
Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.
Mhubiri 3:13 Ecclesiastes 3:13
Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
Mhubiri 3:14 Ecclesiastes 3:14
Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.
Mhubiri 3:15 Ecclesiastes 3:15
Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo yale yaliyopita.
Mhubiri 3:16 Ecclesiastes 3:16
Zaidi ya hayo, nikaona tena chini ya jua ya kwamba, Mahali pa hukumu upo uovu, Na mahali pa haki upo udhalimu.
Mhubiri 3:17 Ecclesiastes 3:17
Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.
Mhubiri 3:18 Ecclesiastes 3:18
Nikasema moyoni mwangu, Ni kwa sababu ya wanadamu, ili Mungu awajaribu, nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama.
Mhubiri 3:19 Ecclesiastes 3:19
Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
Mhubiri 3:20 Ecclesiastes 3:20
Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.
Mhubiri 3:21 Ecclesiastes 3:21
Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?
Mhubiri 3:22 Ecclesiastes 3:22
Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye.