Mhubiri Mlango 3 Ecclesiastes

Mhubiri 3:1 Ecclesiastes 3:1

Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

Mhubiri 3:2 Ecclesiastes 3:2

Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;

Mhubiri 3:3 Ecclesiastes 3:3

Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;

Mhubiri 3:4 Ecclesiastes 3:4

Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;

Mhubiri 3:5 Ecclesiastes 3:5

Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;

Mhubiri 3:6 Ecclesiastes 3:6

Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;

Mhubiri 3:7 Ecclesiastes 3:7

Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

Mhubiri 3:8 Ecclesiastes 3:8

Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.

Mhubiri 3:9 Ecclesiastes 3:9

Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?

Mhubiri 3:10 Ecclesiastes 3:10

Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.

Mhubiri 3:11 Ecclesiastes 3:11

Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.

Mhubiri 3:12 Ecclesiastes 3:12

Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.

Mhubiri 3:13 Ecclesiastes 3:13

Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.

Mhubiri 3:14 Ecclesiastes 3:14

Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.

Mhubiri 3:15 Ecclesiastes 3:15

Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo yale yaliyopita.

Mhubiri 3:16 Ecclesiastes 3:16

Zaidi ya hayo, nikaona tena chini ya jua ya kwamba, Mahali pa hukumu upo uovu, Na mahali pa haki upo udhalimu.

Mhubiri 3:17 Ecclesiastes 3:17

Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.

Mhubiri 3:18 Ecclesiastes 3:18

Nikasema moyoni mwangu, Ni kwa sababu ya wanadamu, ili Mungu awajaribu, nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama.

Mhubiri 3:19 Ecclesiastes 3:19

Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.

Mhubiri 3:20 Ecclesiastes 3:20

Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.

Mhubiri 3:21 Ecclesiastes 3:21

Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?

Mhubiri 3:22 Ecclesiastes 3:22

Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye.